JINSI YAKUBANA NYWELE HALISI, KUTENGENEZA MAWIMBI (NATURAL HAIR)

Kubana nywele kuna kazi haswa kwa wale wenye nywele nyingi, nitaeleza hatua kwa hatua jinsi ya kuzifanya ziwe na mwonekano mzuri na kubana kwa urahisi zaidi. kwanza, zichane nywele zote vizuri mpaka zilainike.Mbili,zigawe mara tatu yaani Kama unabana mabutu (funga na vibanio).Tatu,chukua fundo moja peleka nyuma au hata Kati inategemea na staili unayobana(nyuma,Kati au pembeni).Nne malizia na lile fungu la mwisho kisha zifunge kwa kibanio maalum cha nywele, waweza zungusha mkia au ukaacha hivyo hivyo inategemea utakavyopendelea mwenyewe.kwa wale ambao wangependa kutengeneza mawimbi hatua ya kwanza,chana nywele zako vizuri mpaka zinyooke na uzipake mafuta maalum kwa ajili ya nywele (ya maji au mgando). Pili,kata nywele katika mafungu madogo madogo na kuzisuka mabutu(njia tatu au mbili) ni muhimu kuweka rola kama ukizilowanisha kwa maji kidogoKama unavyoona pichani au usiweke.Tatu,kaa nazo kuanzia SAA moja na kuendelea(ili zikauke vizuri kwa waliotumia rola na maji kidogo) na kwa wale ambao hawata tumia rola waweza lala nazo kama huna mahali pa kwenda kwa muda huo au Kama umefanya usiku.Nne,toa rola(Kama uliweka) na chambua vizuri kwa mkono au chanuo yenye nafasi kubwa ili usiharibu mawimbi ya nywele.

           

No comments:

Post a Comment

Content Copyright © 2016 by Flaviana Maguha All rights reserved.