NGUO ZA KUOGELEA KWA KINA DADA (SWIMING COSTUMES)

Hizi ni nguo maalum zakuogelea na kuendea sehemu za ufukwe nguo hizi mara nyingi huacha sehemu kubwa ya maumbile ya mwanamke wazi ila humfanya awe huru zaidi katika zoezi hilo vilevile hizi ni nguo ambazo maalum zimetengenezwa kwa ajili ya zoezi hilo. Nguo hizi zipo za aina tofauti tofauti zipo chupi na blazia zake na zipo za moja kwa moja kuanzia juu mpka chini yani iliyoungana.inategemea muhusika mwenyewe atapenda nguo zipi Kati ya hizo mbili, lakini pia imekua tofauti kidogo nguo hizo waweza valia suruali au kitu kingine kwa chini haswa zile za moja kwa moja na kuna baadhi ya watu hutumia kufanyia mazoezi haswa wale wanaopendelea kufanya mazoezi ufukweni inakua ikiwapa uhuru zaidi(kama picha zinavyoonyesha)na kwa chupi na blazia kuna baadhi ya watu hutumia Kama nguo za ndani kawaida japo hutegemea zaidi na muundo wa nguo yenyewe na kuna wengine hutumia nguo za ndani walizonazo zinazoendana vizuri nacho sio kitu kibaya. Nguo hizi zinaumuhimu kwa mwanamke kuwa nazo katika kabati lake na tukumbuke kuwa kuogelea hufanya ngozi kuwa nyororo na laini pia hupunguza vipele na harara mwilini na nizoezi tosha kwa watu wasiopenda kufanya mazoezi mengine, ngozi ikiwa laini pia huwezesha vitu vingine Kama mafuta ya mwili kufanya kazi kwa ufasaha na kuleta matokeo mazuri ya ngozi yako. Ikumbukwe kuwa sio kila mtu anaetaka kwenda ufukweni ni lazima kuvaa nguo hizo ni kwa wale wanaoweza tu na haswa kwa sisi watanzania inakua ngumu kidogo kutokana na maadili ya baadhi ya familia zetu japo sio kitu kibaya kufanya cha muhimu kiendane na mazingira halisi ya tendo lenyewe.

No comments:

Post a Comment

Content Copyright © 2016 by Flaviana Maguha All rights reserved.