NYWELE ZA AFRO

Afro ni nywele maarufu zenye muonekano wa kiafrika zaidi, nikimaanisha kuwa waafrika ndo wenye nywele za aina hizi tofauti na watu wa bara la ulaya yani wazungu,nywele hizi hua zinamwonekano wa kujaa zaidi zipo ndefu na fupi pia yani zenye urefu wa kawaida tu,vile vile nywele hizi zipo za kushonea kwa wale ambao hawana aina hii ya nywele lakini pia kuna baadhi ya watu wananywele hizi halisia kabisa yani zisizo za kushonea wala kuvaa. Mara nyingi nywele hizi huwa hazitakiwi kuchanwa haswa zile zisizo halisia yani zakushonea au kuvaa,hupakwa mafuta ya nywele na kuvutwa tu kwa mkono na kukaa sawa lakini kwa wale ambao nizahalisia huchanwa Kama kawaida na haziwezi badilika wala kuharibika kwa sababu ndo uhalisia wake huo.nywele za afro humpendeza kila mtu na hutengenezwa na kubanwa kwa staili mbalimbali inategemea na mtu mwenyewe hupendelea muonekano upi wa nywele zake kwa muda huo, na kwa wale wakutengeneza ambazo sio halisi nywele hizo zipo za rangi tofauti tofauti inategemea na mtu mwenyewe hupendelea vipi. Nywele za aina hii hutumiwa pia na wanaume(kwa nadra Sana) mara nyingi Kama kuna kitu muhimu Kama kurekodi vipindi maalum vya kuchekesha na hata filamu.

No comments:

Post a Comment

Content Copyright © 2016 by Flaviana Maguha All rights reserved.